ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA “TWENZETU KILELENI MSIMU WA 5” NA “TWENZETU SERENGETI”

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA “TWENZETU KILELENI MSIMU WA 5” NA “TWENZETU SERENGETI”



Dar es Salaam, 10 Septemba 2026 Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni za “Twenzetu Kileleni Msimu wa 5” na “Twenzetu Serengeti” katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika National College of Tourism, karibu na IFM City Center, Dar es Salaam.

Kampeni hizo zinalenga kuhamasisha Watanzania, taasisi za Serikali na binafsi, makampuni, mashirika, vyuo, vikundi na jamii kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika utalii wa ndani, huku wakijivunia na kuthamini vivutio vya kipekee ambavyo Tanzania imebarikiwa navyo.

Kupitia Twenzetu Kileleni Msimu wa 5, washiriki watapata fursa ya kupanda Mlima Kilimanjaro kupitia Njia ya Marangu na kufika kileleni tarehe 9 Desemba 2026, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 65 ya Uhuru wa Tanganyika. Gharama maalum ya ushiriki ni Shilingi 1,800,000 kwa mtu, ikijumuisha huduma muhimu za safari kama malazi, chakula, usafiri, tozo za Serikali, huduma za waongoza mlima, wapagazi, wapishi na vifaa muhimu vya kupandia mlima.

Mbali na safari ya kuelekea kileleni, washiriki wa Twenzetu Kileleni pia watapata nafasi ya kupanda miti kama sehemu ya mchango wao katika kuhifadhi mazingira na kuongeza uoto wa asili. Miche hiyo itatolewa na Zara Tanzania Charity, taasisi inayotekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na kimazingira kwa lengo la kusaidia jamii na kuchangia maendeleo endelevu nchini Tanzania.

Hatua hiyo inalenga kuifanya safari ya Twenzetu Kileleni kuwa zaidi ya tukio la kupanda mlima, kwa kuwa washiriki pia wataacha alama chanya katika mazingira kupitia upandaji wa miti na kuhamasisha umuhimu wa utunzaji wa mazingira.



Kwa upande mwingine, Twenzetu Serengeti inalenga kuwapa Watanzania nafasi ya kujionea moja kwa moja utajiri wa wanyamapori na mandhari ya Tanzania kupitia safari inayojumuisha maeneo maarufu ya Tarangire, Serengeti na Ngorongoro.

Gharama ya safari ni Shilingi 1,200,000 kwa mtu, ikiwa ni bei maalum kwa kundi la watu wasiopungua saba.

Safari hiyo inajumuisha malazi, milo, usafiri kwa magari maalum ya safari, viingilio katika hifadhi pamoja na huduma za waongoza wageni wenye uzoefu.


Kupitia kampeni hizi, Zara Tanzania Adventures imeendelea kusisitiza umuhimu wa Watanzania kuwa sehemu ya utalii wa nchi yao badala ya kuishia kusikia au kuona vivutio hivyo kupitia wageni kutoka mataifa mengine.

Taasisi za Serikali, kampuni binafsi, mashirika, vikundi vya kijamii, vyuo na makundi mbalimbali yamehamasishwa kuunda timu na kushiriki katika Twenzetu Kileleni na Twenzetu Serengeti kama mojawapo ya njia za kuonyesha, kuhamasisha na kudumisha uzalendo, kuimarisha mshikamano na kuongeza uelewa kuhusu thamani ya rasilimali za utalii zilizopo nchini.

Ujumbe mkuu wa kampeni hizo ni kuwahamasisha Watanzania kutembelea, kuthamini na kujivunia urithi wao wenyewe.

Desemba hii, tusibaki kusikia habari za Kilimanjaro na Serengeti — twende wenyewe.

Twenzetu Kileleni – Msimu wa 5. Twenzetu Serengeti. Safari ni yetu, Mlima ni wetu, Serengeti ni yetu, Tanzania ni yetu.


Comments

Popular posts from this blog

My biggest achievement is sending people to Kilimanjaro

Tanzania Named Top African Safari Destination by Global Customer Analysis

Kilimanjaro Health Run 2018